KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, March 7, 2012

Mercy auza haki za filamu ya harusi yake

LAGOS, Nigeria
MWIGIZAJI machachari Mercy Johnson ameamua kufuata nyayo za Kim Kardasian kwa kuuza haki za picha za filamu za ndoa yake.
Mercy ameuza haki za filamu hiyo, My Wedding kwa Kampuni ya Great Star Production Ltd.
Filamu hiyo, ambayo ilikuwa izinduliwe Februari 17 mwaka huu, uzinduzi wake umeahirishwa hadi hapo baadaye.
Kuahirishwa kwa uzinduzi huo kumetokana na kampuni ya MJ na ile ya Great Star Production kushindwa kufikia makubaliano ya malipo.
Imedaiwa kuwa, tayari kampuni ya MJ, inayomilikiwa na Mercy, imeshalipwa malipo yote, lakini mwanadada huyo anataka kuhakikishiwa malipo mengine kwa mauzo ya baadaye ya filamu hiyo.

No comments:

Post a Comment