KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, October 31, 2016

BREAKING NEWSSSSS...BONDIA THOMAS MASHALI AFARIKI DUNIA KWA KUSHAMBULIWA NA WATU WASIOJULIKANA



Bondia mtanzania Thomas Mashali maarufu kama (Simba Asiyefugika),amekutwa amekufa huku akiwa na majeraha  usiku wa kuamkia leo huko maeneo ya Kimara jijini Dar es salaam kutokana na sababu ambazo hazijajulikana mpaka sasa.
Kwa mujibu wa katibu mkuu wa Oganization ya ngumi za kulipwa nchini PST Antony  Lutta,ameiambia blogu hii kwamba, taarifa walizozipata ingawa bado  hazijathibitishwa inaonyesha Thomas Mashali ameuwawa.
Lutta ameongeza kwamba marehemu enzi za uhai wake amekuwa na tabia ya kufanya vurugu akiwa amelewa sasa hatujui nini kimempata ambapo  mwili wake umekutwa maeneo ya Kimara jijini Dare s salaam ukiwa na majeraha baada ya hapo  ulichukuliwa na kupelekwa kuhifadhiwa katika  hospitali ya taifa muhimbili.
Marehemu Mashali kabla ya kifo chake alikuwa  acheze na bondia Chimwemwe kutoka nchini Malawi ,pigano ambalo lilipangwa kufanyika mkoani  morogoro siku ambayo bondia mwenzake Dullah Mbabe alipangwa kucheza pigano la utangulizi.
Mashali ambaye  jina lake la  kuzaliwa ni Christopher Fabian Mashali,aliyezaliwa Septemba 09 mwaka 1989,ameacha rekodi ya kushinda mapambano 19 kati ya hayo 9 akishinda kwa KO,amepoteza mapambano 5 kati ya hayo amepigwa kwa KO mapambano 4 huku akitoka sare pigano moja tu.
Marehemu ameacha mke na watoto

1 comment:

  1. Hello, Je, unahitaji mkopo kutoka kampuni kuaminiwa zaidi na ya kuaminika
    katika dunia? kama ndiyo basi wasiliana nasi sasa kwa sisi kutoa mkopo kwa wote
    makundi ya watu wanaotafuta kuwa ni makampuni au kwa ajili ya matumizi ya wafanyakazi. Tunatoa
    mkopo kwa kiwango 3% riba, Wasiliana nasi kupitia barua pepe:
    jonsonlanld@gmail.com

    (1) Jina kamili
    (2) Full mitaani
    (3) Nchi
    (4) Umri
    (5) Kazi
    (6) Mwambie namba ya simu
    (7) Jinsia:
    (8) Loan Kiasi inahitajika:
    (9) Loan Duration

    Email yetu katika: jonsonlanld@gmail.com

    ReplyDelete