KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, October 3, 2016

NDOTO YA SERENGETI BOYS KUFUZU KUCHEZA FAINALI ZA AFRIKA YAOTA MBAWA, YACHAPWA BAO 1-0 NA CONGO BRAZZAVILLE



NDOTO za timu ya soka ya Taifa ya vijana wa chini ya miaka 17, Serengeti Boys kufuzu kucheza fainali za Afrika mwakani, zimeota mbawa baada ya kuchapwa bao 1-0 na Congo Brazzavile.

Katika mechi hiyo ya marudiano iliyochezwa jana mjini Librevvile, Serengeti Boys ilikuwa ikihitaji sare ya aina yoyote ili iweze kusonga mbele.

Kutokana na kipigo hicho, Congo imefuzu kucheza fainali hizo kutokana na faida ya mabao ya ugenini, baada ya matokeo ya jumla kuwa sare ya mabao 3-3.

Katika mechi ya awali iliyochezwa wiki mbili zilizopita mjini Dar es Salaam, Serengeti Boys iliichapa Congo mabao 3-2.

No comments:

Post a Comment