KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, October 23, 2016

YANGA YATOA DOZI KALI KWA KAGERA SUGAR, YAIKUNG'UTA MABAO 6-2







YANGA sasa imeanza kuonyesha cheche zake katika michuano ya ligi kuu ya Tanzania Bara baada ya kuibugiza Kagera Sugar mabao 6-2 kwenye Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba.

Ushindi huo, ambao ni wa kwanza mkubwa kwa Yanga tangu ligi hiyo ilipoanza, umeiwezesha Yanga kuchupa hadi nafasi ya pili, ikiwa na pointi 21 baada ya kucheza mechi 10, nyuma ya Simba inayoongoza kwa kuwa na pointi 26.

Katika mechi hiyo iliyokuwa na ushindani mkali kipindi cha kwanza, hadi kilipomalizika Yanga ilikuwa mbele kwa mabao 3-1.

Kagera Sugar ilikuwa ya kwanza kufunga bao dakika ya tatu lililopachikwa wavuni na Mbaraka Yussuf kabla ya Donald Ngoma kuisawazishia Yanga dakika ya nne.

Simon Msuva aliiongezea Yanga bao la pili dakika ya 21 kabla ya Obrey Chirwa kufunga la tatu dakika ya 26.

Kagera ilikianza kipindi cha pili kwa kasi na kuongeza bao la pili dakika ya 49 lililofungwa tena na Mbaraka kabla ya Yanga kuongeza mabao mengine matatu kupitia kwa Deus Kaseke, Chirwa na Ngoma.

Katika mechi nyingine ya ligi hiyo iliyochezwa jana, Azam ilizinduka toka usingizini baada ya kuichaa JKTRuvu bao 1-0 kwenye Uwanja wa Chamazi Complex, Dar es Salaam.

Bao pekee na la ushindi la Azam lilifungwa na nahodha wake, John Bocco kwa njia ya penalti dakika ya 57.

No comments:

Post a Comment