KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, October 31, 2016

MREMBO WA TANZANIA 2016 AKANA KUWA NA SHAHADA YA CHUO KIKUU



Diana ameamua kuweka kila kitu wazi kwa kusema: ‘Jina langu ni Diana Loi Lukumay, mmasai na umri wangu ni miaka 18, nilizaliwa Arusha Mount Meru Hospital na ni mtoto wa tatu kwenye familia ya watoto wanne’

‘Nilisoma shule ya msingi ya serikali Levolosi 2005-2011, sekondari ya kutwa ya serikali Arusha 2012 -2015,  matokeo ya kidato cha nne nilipata darala la pili… nilichaguliwa kujiunga na kidato cha tano mchepuo wa Sanaa kwenda shule ya Wasichana Bwiru Mwanza‘

‘Kwakuwa nilikua tayari nipo kwenye tasnia ya urembo niliamua kutojiunga na masomo hayo kwakuwa yalishaingiliana na ratiba za mashindano haya katika ngazi ya kitongoji ambapo nilijiunga na kambi ya Miss Ubungo 2016/2017)‘ – Diana

‘Baada ya kuahirisha masomo ya kidato cha tano niliomba kujiunga na masomo ya ngazi ya cheti kozi ya maswala ya kodi katika chuo cha usimamizi wa fedha ambapo mpaka masomo yanaanza mwanzoni mwa October 2016 tayari nilikua kwenye kambi ya Miss Tanzania, mafanikio ambayo niliyapata baada ya kuibuka mshindi na kutangazwa kuwa lete Raha Miss Kinondoni 2016/2017′

‘Juhudi zangu hazikuishia hapo, nilipotangazwa mshindi sikubweteka na taji hilo bali niliendelea na kazi zangu za kijamii katika jamii yangu ya kimasai‘ – Diana

No comments:

Post a Comment