KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Saturday, October 29, 2016

LIGI YA WANAWAKE KUCHEZESHWA NA WAAMUZI WA KIKE



WAAMUZI wa kike ndiyo watakaopewa nafasi zaidi kuchezesha Ligi ya soka la Wanawake Tanzania, inayotarajiwa kuzinduliwa rasmi Novemba Mosi katika Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma huku viwanja vitatu vikitarajiwa kuwaka moto.
Hayo yamesemea na Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Alfred Lucas alipokuwa anazungumza na Waandishi wa Habari leo mjini Dar es Saaalam jana Dar es Salaam.
Ligi huyo inayotarajiwa kuanza Novemba 1, mwaka huu kuwa wanaamini katika uzinduzi huo utakuwa wa pekee kwa sababu utahudhuriwa na wabunge wa Bunge la Tanzania.
Ligi hiyo ambayo inatarajiwa kuwa na ushindani kutokana na kuwakikishwa na nyota mbalimbali kutoka mikoa mbalimbali Tanzania Bara imegawanyika katika makundi A na Bekee kwa sababu utahudhuriwa na wabunge wa Bunge la Tanzania.
Alizitaja timu ambazo zitafungua ligi hiyo kuwa ni Baobao Queens ya Dodoma itawakaribisha Victoria ya Iringa mchezo ambao utacgezwa uwanja wa Jamhuri Dodoma, Marsh ya Mwanza itakuwa wageni wa Majengo ya Kigoma Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza.
Mchezo mwingine utakuwa katika Uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam ambapo wenyeji JKT Queens watakuwa wenyeji wa Mlandizi Queens.
Alisema kuwa benchi la ufundi la timu ya taifa ya wanawake, litagawanywa katika mikoa hiyo ili kuangalia wachezaji wenye uwezo ambao wataunda kwenye kikosi cha timu ya taifa.
"Timu ya taifa itatolewa na mashindano haya, hatutakuwa na wachezaji wale wale kila siku na pia ligi hii itatisaidia kupata kikosi cha vijana U-20," alisema.

No comments:

Post a Comment