KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, October 3, 2016

AZAM YALAZIMISHWA SARE NA RUVU SHOOTING



AZAM FC imelazimishwa sare ya kufungana mabao 2-2 na Ruvu Shooting katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara usiku wa leo Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.
Matokeo hayo yanaifanya Azam FC ifikishe pointi 11 baada ya kucheza mechi saba, ikishinda tatu, sare mbili na kufungwa mbili.
Ruvu Shooting inafikisha pointi tisa baada ya kucheza mechi saba, ikishinda mbili, kufungwa mbili na sare tatu.
Fullyuzulu Maganga alianza kuifungia Ruvu dakika ya nane, kabla ya Jean Baptiste Mugiraneza kuisawazishia Azam FC dakika ya 46 akimalizia kona ya Khamis Mcha ‘Vialli’.
Mcha akaifungia bao la pili Azam FC dakika ya 70, kabla ya mkongwe Shaaban Kisiga ‘Malone’ kuifunga timu yake ya zamani dakika ya 89 akiisawazishia Ruvu Shooting. 
Mechi nyingine za Ligi Kuu leo, Mbeya City imeshinda 1-0 dhidi ya Mwadui FC Uwanja wa Sokoine, Mbeya bao pekee la Ditram Nchimbi, wakati Mbao FC imelazimishwa sare ya 0-0 na JKT Ruvu Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza, wakati Maji Maji imefungwa nyumbani 2-0 na Stand United mjini Songea.

No comments:

Post a Comment