KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Saturday, October 29, 2016

SERIKALI YAMREJESHA PLUIJM YANGA



HATIMAYE klabu ya Yanga imeamua kubadili gea angani kwa kumuandikia barua Kocha wake, Hans van der Pluijm, kumtaka abadili uamuzi wake wa kujiuzulu kuifundisha timu hiyo.

Barua hiyo iliyotiwa saini na Katibu Mkuu wa Yanga, Baraka Deusdedit, imeeleza kuwa hawaoni sababu ya kuachana na Pluijm baada ya kuwa ameiletea mafanikio makubwa timu hiyo.
 
Kocha huyo kutoka Uholanzi, alijiuzulu mapema wiki hii baada ya kukerwa na uongozi wa Yanga, kumleta kocha mpya, George Lwandamina kutoka Zambia bila kumtaarifu, akisema huko ni kumvunjia heshima.

Aidha, Pluijm alikataa kutumikia wadhifa wa mkurugenzi wa ufundi, ambao Yanga ilimtunukia baada ya kumleta Lwandamina kuwa kocha mkuu.

Hatua hiyo ya Yanga kumrejesha Pluijm imekuja baada ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba, kuamua kuingilia kati sakata hilo.

Waziri huyo kijana, ambaye ni mwanachama wa Yanga, aliushauri uongozi wa Yanga kumrejesha Pluijm na baadaye kumshawishi kocha huyo abadili uamuzi wake.

No comments:

Post a Comment