KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Saturday, October 8, 2016

MATAJIRI WA KIARABU KUONGOZA KAMATI YA MASHINDANO SIMBA




KLABU ya Simba SC ya Dar es Salaam imeunda Kamati mpya ya Mashindano, ambayo itakuwa chini ya Watanzania kadhaa wenye asili ya Kiarabu, akiwemo Mwenyekiti, Musley Al Ruwah.
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano ya Simba SC, Haji Sunday Manara amesema leo Dar es Salaam katika Mkutano na Waandishi wa habari kwamba Kamati hiyo imeundwa ili kuongeza nguvu katika vita ya ubingwa wa Ligi Kuu.
Na Manara, motto wa kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Sunday Manara ‘Kompyuta’ amewataka watu wengine katika Kamati hiyo, ni Makamu Mwenyekiti, Alhaj Hassan Hassanoo na Wajumbe; Mohamed Nassor wenye asili ya Kiarabu pia, Cossmas Kapinga, Juma Pinto na Octavian Mushi.
Katika hatua nyingine, Manara amesema kwamba Simba imemuandikia barua Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo, Nape Moses Nnauye kumuomba awaombee msamaha kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Pombe Joseph Magufuli waruhusiwe kuendendelea kutumia Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Manara alisema kwamba wameona umuhimu wa kuomba radhi kwa kitendo cha mashabiki wachache kuharibu raslimali ambazo zimejengwa kwa kodi za Watanzania wote.
“Rais ndiye msimamizi wa raslimali za nchi hii, hivyo tumemuandikia barua Waziri Nape kumuomba atuombee radhi kwa Rais Magufuli, kwa kitendo cha mashabiki wetu kung’oa vitu kwenye mchezo wa Oktoba 1 (2016) dhidi ya Yanga”, alisema Manara.
“Wakati tukiwa jukwaa kuu na kuona tukio lile likitendeka, tulitamani kuruka kwenda kuwazuia mashabiki wasing’oe viti, lakini hatukuweza, ilikuwa mbali, lakini tunaaahidi tukio kama lile halitatokea tena, kwani limeshusha thamani ya klabu yetu,”alisema.
Aidha, Manara ameiomba Serikali kupitia Menejimenti ya Uwanja wa Taifa kufunga kamera ili kunasa matukio kwa lengo la kuwabaini wahusika wa uharibifu. Akawaomba pia askari Polisi wanaopangiwa kusimamia usalama uwanjani kuhakikisha wanawatazama mashabiki badala ya kuangalia mchezo ili kujiweka tayari kupambana na wahalifu.

No comments:

Post a Comment