KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, October 31, 2016

YANGA YAIFUMUA MBAO FC MABAO 3-0



YANGA leo imemrejesha Kocha wake, Hans van der Pluijm kwa furaha baada ya kuitandika Mbao FC mabao 3-0 katika mechi ya ligi kuu iliyochezwa kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.

Kutokana na ushindi huo, Yanga sasa imefikisha pointi 27 baada ya kucheza mechi 12, ikiwa kwenye nafasi ya pili nyuma ya Simba, inayoongoza kwa kuwa na pointi 32.

Mabao yaliyoiwezesha Yanga kutoka uwanjani na pointi zote tatu yalifungwa na beki Vicent Bossou, Mbuyu Twite na Amisi Tambwe.

Licha ya Yanga kuibuka na ushindi huo mnono wa mabao, timu hizo zilimaliza kipindi cha kwanza zikiwa suluhu, huku kila moja ikiwa imeonyesha uwezo mkubwa.

No comments:

Post a Comment