KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, October 19, 2016

YANGA, TOTO AFRICAN DIMBANI LEO MWANZA, SIMBA NA MBAO FC KESHO DAR



Michezo sita ya ligi kuu ya Tanzania Bara, inatarajiwa kufanyika leo Jumatano, Oktoba 19, mwaka huu, likiwemo pambano kati ya Yanga na Toto African.

Vodacom – Kampuni ya simu za mkononi inayoongoza nchini kwa kutoa huduma za kisasa za mawasiliano ndiyo mdhamini mkuu ligi hiyo ikisaidiana kwa karibu sana Kampuni ya kisasa ya vyombo vya habari yenye kurusha vipindi vyake kwa weledi na ubora wa hali ya juu ya Azam Televisheni (Azam Tv) na DTB- Benki ya kuaminika nchini kwa usalama wa fedha zako.

Kampuni hizo zinazong’arisha VPL, kesho zitakuwa sambamba kwenye kuchagiza michezo ya Ruvu Shooting ya Pwani ambayo itaikaribisha Mwadui ya Shinyanga kwenye Uwanja wa Mabatini uliuoko Mlandizi mkoani Pwani katika mchezo Na. 81 wa VPL utakaoanza saa 10.00 jioni.

Mchezo Na. 82 utakaozikutanisha Azam FC ya Dar es Salaam na Mtibwa Sugar ya Morogoro utafanyika saa 1.00 usiku (19h00). Mchezo huo utafanyika Uwanja wa Azam ulioko Chamazi – maskani ya Azam yalioko nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam wakati mchezo Na. 83 utazikutanisha timu za Ndanda FC na Mbeya City ya Mbeya kwenye Uwanja wa Nangwanda Sijaona mjini Mtwara.

Mchezo Na. 85 utazikutanisha timu za Tanzania Prisons ya Mbeya na Stand United itakayokuwa mgeni kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya huku mechi Na. 87 itazikutanisha Toto African ya Mwanza itakayocheza na Young Africans kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza wakati African Lyon itakuwa mwenyeji wa Majimaji ya Songea kwenye Uwanja wa Uhuru, jijini Dar es Salaam kwenye mchezo Na. 88.

Ligi hiyo itaendelea tena kesho Alhamisi Oktoba 20, kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam ambako vinara wa ligi hiyo kwenye msimamo hadi sasa, Simba itakuwa mwenyeji wa Mbao FC ya Mwanza katika mchezo Na. 84.

No comments:

Post a Comment