KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, October 31, 2016

ALICHOSEMA FARAJA KOTTA KUHUSU MREMBO WA TANZANIA 2016



Niliposhinda Miss Tanzania, kuna mtangazaji fulani (tena wa kiume) wa kipindi cha redio cha asubuhi alitumia kama saa nzima hewani kusema ambavyo sikustahili kushinda. Asubuhi ya Jumatatu kama leo baada ya weekend ya shindano. Nilipigiwa simu kuamshwa. Nakumbuka niliamka nikawasha redio na nikasikiliza kipindi chote, peke yangu, chumbani. Nilitetemeka, nilishindwa kuoga, kula, nilijifungia ndani siku nzima nikilia. Niliwaza sana ambavyo pengine ni kweli sikustahili. Nilijuta kushiriki Miss Tanzania. I was young and naive. I had just turned 19, coming straight from the safety nets of Catholic nuns boarding schools. Sikujua kuna watu wanaweza kuwa na roho mbaya hata kwa watu wasiowajua. It took my parents (RIP) na kila busara waliyonayo kunifanya nijisikie vizuri. I had to dig deep inside me to regain my purpose. I was exposed to a cruel world and yes, I quickly learnt, it is what it is. Leo hii hakuna binadamu mwenye hiyo nguvu niliyompa yule mtangazaji. I learnt the hard way but I am grateful for the lesson. Thank God I learnt early. Kuna sehemu ya nguvu niliyo nayo leo iliyotokana na kujeruhiwa na binadamu na kupona. Lakini si kila mtu atapata bahati ya kupona, unaweza kumjeruhi mtu na akapotea moja kwa moja. Usijitafutie laana za reja reja. To the newly crowned Miss Tanzania, Do you honey! To the rest of us, tujenge zaidi ya kubomoa. Love doesn't cost a thing! God bless, Faraja 


No comments:

Post a Comment