KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, October 19, 2016

LIGI DARAJA LA PILI KUANZA OKTOBA 29




Timu 24, zinatarajiwa kupambana katika michuano ya Ligi Daraja la Pili msimu wa 2016/17 kuanzia Oktoba 29, mwaka huu, imefahamika.

Timu hizo zimepangwa katika makundi manne yenye timu sita kwa kuangalia zaidi jiografia au kanda ambako timu imetoka – lengo likiwa kupunguza gharama kwa timu shiriki hasa ikizingatiwa kuwa michuano hiyo haijapata mdhamini hadi sasa.

Kundi A lina timu za Mashujaa ya Kigoma, Mirambo ya Tabora, Mji Mkuu ya Dodoma, Green Warriors ya Pwani, Bulyanhulu na Transit Camp za Shinyanga.

Mechi za kwanza zitakuwa ni kati ya Mashujaa dhidi ya Green kwenye Uwanja wa Tanganyika mjini Kigoma wakati Mirambo itaikaribisha Mji Mkuu kwenye Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi. Timu za Transit Camp na Bulyanhulu zitacheza Oktoba 30, mwaka huu.

Kundi B; African Wanderers ya Iringa itaikaribisha AFC ya Arusha kwenye Uwanja wa Kichangani mjini Iringa siku ya Oktoba 29, 2016 wakati Kitayosa itakuwa mgeni wa Madini kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha. Timu nyingine kwenye kundi hilo ni Pepsi ambayo itacheza na JKT Oljoro Oktoba 30, mwaka huu.

Kundi C; Villa Squad itafungua dimba na Kariakoo ya Lindi kwenye Uwanja wa Karume, Ilala jijini Dar es Salaam wakati Burkinafaso ya itaikaribisha Abajalo kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro. Timu nyingine kwenye kundi hilo ni Cchanganyikeni na Cosmopolitan za Dar es Salaam.

Kundi D; Namungo ya Lindi itafungua dimba na Sabasaba kwenye Uwanja wa Sokoine ulioko Nachingwea mkoani Lindi wakati Mkamba Rangers itakuwa nyumbani kwenye Uwanja wa Mkamba kuikaribisha Mawenzi Market kwenye Uwanja wa Mkamba ulioko Morogoro.

No comments:

Post a Comment