KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Saturday, October 29, 2016

YANGA YAIGAGADUA JKT RUVU 4-0




YANGA jana iliendelea kung'ara katika michuano ya soka ya ligi kuu ya Tanzania Bara baada ya kuibugiza JKT Ruvu mabao 4-0.

Katika mechi hiyo iliyochezwa kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam, Yanga ilijipatia mabao hayo manne kupitia kwa washambuliaji wake, Amis Tambwe, aliyefunga mawili, Obrey Chirwa na Simon Msuva.

Yanga ilicheza mechi hiyo ikiwa chini ya kocha wake msaidizi, Juma Mwambusi, baada ya Kocha Mkuu, Hans van der Pluijm kutangaza kujiuzulu.

Kutokana na ushindi huo, Yanga imeendelea kujichimbia nafasi ya pili katika msimamo wa ligi hiyo, ikiwa nyuma ya watani wao Simba kwa tofauti ya pointi moja.

No comments:

Post a Comment