KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Saturday, October 29, 2016

BOCCO AITOA KIMASOMASO AZAM


AZAM jana iliendelea kujitutumua katika michuano ya ligi kuu ya Tanzania Bara, baada ya kuitandika Kagera Sugar mabao 3-2 kwenye Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba.

Mshambuliaji na nahodha John Bocco ndiye aliyeiwezesha Azam kutoka uwanjani na pointi zote tatu baada ya kuifungia bao la ushindi zikiwa zimesalia dakika nne kabla ya pambano hilo kumalizika.

Ushindi huo ulikuwa wa pili mfululizo kwa Azam baada ya kupokea vipigo katika mechi zake zilizopita huku ikiwa imejikusanyia poiti 19 baada ya kucheza mechi 12.

Kagera ilikuwa ya kwanza kupata bao dakika ya 32 kupitia kwa Themi Felix kabla ya Mudathir Yahya kuisawazishia Azam dakika tano zilizofuata. Mabao hayo yalidumu hadi mapumziko.

Felix aliiongezea Kagera bao la pili kwa njia ya penalti baada ya beki Aggrey Morris wa Azam kumchezea rafu Ally Nassoro ndani ya eneo la hatari.

Frank Domayo aliisawazishia Azam dakika ya 80 kwa shuti kali baada ya kipa wa Kagera kutema shuti la Bocco.

No comments:

Post a Comment