KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, October 23, 2016

MKUTANO MKUU WA DHARULA YANGA WAOTA MBAWA



MWENYEKITI wa Yanga, Yussuf Manji ametii agizo la Mahakama kwa kuufuta Mkutano Mkuu wa dharula wa klabu ya Yanga uliopangwa kufanyika kesho makao makuu ya klabu, Jangwani, Dar es Salaam.
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam jana ilitoa katazo la kufanyika Mkutano wa kesho kufutia kesi iliyofunguliwa na baadhi ya wanachama wa klabu hiyo.
Manji ametangaza kuufuta Mkutano huo mchana wa leo akizungumza na Waandishi wa Habari Jangwani.
Na amesema taratibu za kisheria zinafanyika juu ya kupambana na pingamizi hilo ili liondolewe na tarehe nyingine ya Mkutano itatajawa mara mpango huo utakapofanikiwa.
Kwa mujibu wa hati ya agizo halali la Mahakama, uongozi wa Yanga umezuiwa kufanya Mkutano huo baada ya kesi iliyofunguliwa mahakamani hapo dhidi ya Mwenyekiti wa klabu, Yussuf Manji na Kampuni ya Yanga Yetu.
Ajenda kuu ya Mkutano huo ilikuwa ni kupitisha Baraza la Wadhamini la klabu hiyo pamoja na kuondoa Mjumbe mmoja na kuweka mpya.
Na hayo yanafuatia Baraza la Wadhamini kuikodisha timu kwa kampuni ya Yanga Yetu kwa miaka 10, baada ya wanachama kuafiki ombi la Mwenyekiti wao, Yussuf Manji katika Mkutano wa Agosti 6, mwaka huu.

No comments:

Post a Comment