KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, October 24, 2016

SIMBA YAIBUGIZA TOTO AFRICAN 3-0




SIMBA jana iliendeleza wimbi la ushindi katika michuano ya soka ya ligi kuu ya Tanzania Bara, baada ya kuibugiza Toto African mabao 3-0.

Katika mechi hiyo iliyochezwa kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam, Simba ilikwenda mapumziko ikiwa mbele kwa bao 1-0.

Kutokana na ushindi huo, Simba sasa inazo pointi 29 baada ya kucheza mechi 11, ikifuatiwa na Yanga yenye pointi 21 baada ya kucheza mechi 10.

Mshambuliaji Muzamil Yassin aliifungia Simba bao la kuongoza dakika ya 42 baada ya kupokea pasi safi kutoka kwa Frederick Blagnon.

Mrundi Laudit Mavugo aliiongezea Simba bao la pili dakika ya 51 baada ya kutengenezewa chumba safi na Muzamil.

Zikiwa zimesalia dakika 16 pambano hilo kumalizika, Muzamil aliiongezea Simba bao la tatu baada ya kumalizia kona iliyochongwa na Shiza Kichuya.

No comments:

Post a Comment