KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, October 3, 2016

WASANII NCHINI WAMETAKIWA KUTUMIA SANAA ZAO KUELIMISHA JAMII KUFANYA KAZI KWA BIDII.

Kaimu Mkurugenzi Idara ya Maendeleo ya Sanaa kutoka Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Bibi Leah Kihimbi akizungumza na wananchi pamoja na wasanii mbalimbali (hawapo pichani) wakati alipokua anafunga Tamasha la 35 la Sanaa na Utamaduni Bagamoyo lilioandaliwa na Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) Wilayani Bagamoyo Oktoba mosi.
Mtendaji Mkuu wa  Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) Dkt. Herbet Makoye akitoa hotuba kwa wananchi pamoja na wasanii mbalimbali (hawapo pichani) wakati  Tamasha la 35 la Sanaa na Utamaduni Bagamoyo lilioandaliwa na Taasisi  hiyo  lilipofungwa rasmi Wilayani  Bagamoyo Oktoba mosi.
Vikundi mbalimbali vya burudani  kutoka Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) vikitoa burudani kwa  wananchi  pamoja na wasanii  mbalimbali (hawapo pichani) katika ufungaji wa Tamasha la 35  la Sanaa na Utamaduni  Bagamoyo  lilioandaliwa  na Taasisi  hiyo   Wilayani  Bagamoyo Oktoba mosi.


Kaimu Mkurugenzi Idara ya Maendeleo ya Sanaa kutoka Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Bibi Leah Kihimbi akiangalia bidhaa za urembo kutoka kwa mbunifu Mariam Kiiza kabla ya kufunga   Tamasha la 35 la Sanaa na Utamaduni Bagamoyo  lilioandaliwa na Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) Wilayani Bagamoyo Oktoba mosi.
Baadhi ya wanachi walioshiriki ufungaji wa Tamasha la 35 la Sanaa na Utamaduni  Bagamoyo  lilioandaliwa  na Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa)  Wilayani Bagamoyo Oktoba mosi.
 

Na  Shamimu  Nyaki-WHUSM.

Katika kuhakikisha Watanzania wanafanya kazi kwa maendeleo yao na Taifa nchini Serikali imewataka wasanii mbalimbali kutumia Sanaa yao kuelimisha jamii umuhimu wa kufanya kazi kwa bidii.

Wito huo umetolewa jana Wilayani  Bagamoyo  na Katibu Mkuu Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na  Michezo  Prof. Elisante Ole Gabriel  katika hotuba yake ya kufunga Tamasha la 35 la Sanaa na Utamaduni Bagamoyo lililoandaliwa na Taasisi ya Sanaana Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa).

Katibu Mkuu katika hotuba yake iliyosomwa na Kaimu Mkurugenzi  Idara ya Maendeleo ya Sanaa ya Wizara hiyo Bibi. Leah Kihimbi amesema kuwa Wasanii wana nafasi kubwa ya kufikia Watanzania wengi kutokana  na kazi zao hivyo watumie nafasi  hiyo kutoa elimu kwa jamii kuhusu umuhimu wa Kufanya kazi.

“Wasanii  mkidhamiria jambo hufanyika  na uwezo wa kufanya hivyo mnao,ni vizuri mkatumia Sanaa yenu kuwaelimisha wanachi  manufaa ya kufanya kazi kwao wenyewe na Taifa kwa ujumla”.Alisema Prof.Ole Gabriel.

Kwa upande wake Mtendaji  Mkuu wa  Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa) Dkt. Herbet  Makoye mbali na kuwashukuru  wasanii wote waliohudhuria  Tamasha hilo amewataka  pia waendelee kufanya Sanaa zenye ubora na zinazoitangaza Tanzania Ulimwenguni.

“Mmeshiriki vizuri katika Tamasha hili niwasihi muendelee kufanya Sanaa iliyo bora inayotangaza nchi yetu kote  Ulimwenguni ukizingatia tunazo Sanaa za aina mbalimbali ikiwemo ngoma,muziki,filamu na sanaa za ufundi”.Aliongeza Dkt.Makoye.

Aidha msanii  Ebeneza Lukas anaefanya muziki amesemaTamasha limempa ujuzi na weledi mkubwa katika Sanaa yake ukizingatia kuwa yeye ndio anaanza kufanya Sanaa.

Tamasha hilo lililofunguliwa Septemba 26 mwaka huu na Naibu Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa naMichezo Mhe.Anastazia Wambura  limefungwa Oktoba mosi ambapo kazi mbalimbali za Sanaa zilifanyika ikiwa ni pamoja na  makongamano  na warsha mbalimbali.

No comments:

Post a Comment