KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Friday, May 18, 2012

Uche Jombo afunga ndoa kwa siri


LAGOS, Nigeria
HATIMAYE mcheza filamu machachari wa Nigeria, Uche Jombo anadaiwa kufunga ndoa kwa siri na rafiki yake wa Kimarekani.
Uche anadaiwa kufunga ndoa hiyo mwishoni mwa wiki iliyopita katika Jiji la New York nchini Marekani.
Awali, kulikuwa na uvumi kwamba Uche alipanga kufunga ndoa hivi karibuni na kijana huyo hivi karibuni.
Lakini Uche alikanusha uvumi huo kwa kusema, hana mpango wa kufunga ndoa na Mmarekani huyo.
Hata hivyo, kwa mshangao wa wengi, habari za uhakika kutoka kwa watu wa karibu na mwigizaji huyo zimeeleza kuwa, tayari ameshafunga ndoa na kijana huyo.
Kwa sasa, Uche na mumewe huyo wapo fungate nchini Marekani.

No comments:

Post a Comment