KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Friday, May 18, 2012

Aki amwacha solemba mkewe?



LAGOS, Nigeria
MWIGIZAJI nyota wa filamu nchini Nigeria, Chinedu Ikedieze (Aki) amedaiwa kumwacha solemba mkewe, Nneoma Nwaijah.
Tetesi za Aki kumwacha solemba mkewe, zilianza kuvuma mwezi uliopita baada ya mcheza filamu huyo kuonekana akihudhuria sherehe za utoaji wa tuzo za waigizaji bora akiwa na wanawake watano.
Katika sherehe hizo zilizofanyika kwenye hoteli ya Eko mjini Lagos, Aki alifika ukumbini bila ya mkewe.
Uamuzi wa Aki kutofuatana na mkewe kwenye sherehe hizo uliwaacha vinywa wazi watu wengi, hasa katika kipindi hiki, ambacho ndio yao bado ina miezi michache.
Baadhi ya wadau wa tasnia ya filamu walitarajia kumuona Aki akiwa amefuatana na Nneoma, ikiwa ni ishara ya kukoleza penzi lao.
Badala yake, Aki alitinga ukumbini akiwa ameongozana na wanawake watano, ambao walikuwa na miili mikubwa kuliko mkewe.
Tukio hilo lilitafsiriwa na baadhi ya wadau hao kuwa, huenda Aki ametengana na mkewe ama kuna tatizo limetokea kati yao.
Hata hivyo, mmoja wa watu wa karibu na mwigizaji huyo aliueleza mtandao wa naijerules kuwa, Nneoma hapendi kujirusha.
“Naweza kukuhakikishia kwamba, hakuna tatizo lolote kati ya wanandoa hao. Nneoma si aina ya mtu anayependa kujirusha,”alisema mtu huyo.
Aki na Nneoma walifunga ndoa Desemba 9 mwaka jana . Walianza kufunga ndoa ya kimila huko Obolo, Isiala Mbano katika jimbo la Imo na kufuatiwa na ndoa ya kanisani iliyofungwa mjini Lagos.

No comments:

Post a Comment