KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Tuesday, May 8, 2012

Taifa Queens yaanza kwa kishindo kuwania ubingwa wa Afrika


TIMU ya taifa ya netiboli ya Tanzania, Taifa Queens, leo imeanza vema mashindano ya Afrika baada ya kuichapa timu ya Lesotho kwa magoli 57-13, katika mechi ya ufunguzi iliyorindima kwenye Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam.

Katika mchezo huo, Taifa Queens ikiongozwa na wafungaji wake, Mwanaidi Hassan ‘Pereirra’ (GS) na Irene Elias (GA), ambao walikuwa wakiunganishwa vema na kiungo, Faraja Malaki (C), Evodia Kazinja (WA), na Restuta Boniface (WD), hadi robo ya kwanza inamalizika, walikuwa mbele kwa magoli 13-3.

Robo ya pili, Taifa Queens ilizidi kuchanua mbele ya mgeni rasmi, Mke wa Rais Kikwete, Mama Salma, ambapo hadi inamalizika walitoka na magoli 23-9 huku robo tatu wakimaliza kwa 40-13.

Robo ya nne, ukuta wa Taifa Queens uliokuwa chini ya Lilian Sylidion (GD), na Doritha Mbunda (GK), uliwabana vilivyo wafungaji wa Lesotho na hadi mchezo unamalizika, waliibuka kidedea kwa ushindi huo wa magoli 57-13.

Michuano hiyo inayoshirikisha nchi nane, inaendelea tena leo kwa mechi kati ya Botswana na Zambia, Malawi na Zimbabwe, huku wenyeji Tanzania wakitupa karata tena kwa Zambia.

No comments:

Post a Comment