KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, May 3, 2012

Swahiba wa Kanumba aacha uigizaji filamu


LAGOS, Nigeria
MCHEZA filamu nyota wa Nigeria, Ramsey Nouah amesema anatarajia kuacha uigizaji hivi karibuni baada ya kuwepo kwenye tasnia hiyo kwa miaka kadhaa.
Ramsey, ambaye ni swahiba mkubwa wa aliyekuwa mwigizaji nyota wa Tanzania, marehemu Steven Kanumba alisema wiki hii kuwa, amefikia uamuzi huo baada ya kuona inatosha.
Nyota huyo mwenye sura yenye mvuto alisema, ameona ni bora kuachia ngazi akiwa bado kwenye kiwango cha juu badala ya kusubiri fani hiyo imtupe mkono.
“Kwa mashabiki wangi na wengine, naelewa siku zote wanataka kuniona kwenye luninga, lakini kama waswahili wanavyosema, ni bora kuondoka wakati bado upo juu,”alisema.
Ramsey alisema anaamini ameacha kumbukumbu kubwa katika uigizaji na kuongeza kuwa ni vigumu kuzungumzia Nollywood bila kutaja jina lake.
Alisema kwa kipindi kirefu sasa hajacheza filamu yoyote kwa sababu hataki kuonekana kwenye luninga. Alisema anachotaka ni kucheza filamu za kiwango cha juu na zitakazoiweka fani hiyo nchini Nigeria kwenye hatua za juu zaidi.
Alisema baada ya kustaafu kazi hiyo, anatarajia kuwa mwongozaji wa filamu. Alisema asingependa kuwaona watoto wake wakijihusisha na fani hiyo, lakini hawezi kuwalazimisha.

No comments:

Post a Comment