KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, May 7, 2012

Maandalizi tuzo za TASWA yaanza


CHAMA Cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA), kimeanza mchakato wa Tuzo kwa
Wanamichezo Bora wa Tanzania mwaka 2011.
Katibu Mkuu wa TASWA, Amir Mhando ameiambia BIN ZUBEIRY leo kwamba kama
ilivyokuwa mwaka uliopita Kamati ya Utendaji ya TASWA imeamua suala la mchakato wa kuwapata
wanamichezo hao lifanywe na kamati maalum nje ya Kamati ya Utendaji ya TASWA lengo ikiwa ni
kupanua wigo na kuwashirikisha wadau wengi zaidi katika jambo hili nyeti.Kutokana na hali hiyo Kamati
ya Utendaji ya TASWA imeshateua kamati maalum ya kusimamia tuzo hiyo, ambapo kamati hiyo
ambayo tayari imeshaanza vikao vyake jijini Dar es Salaam ipo chini ya Mhariri Mkuu wa gazeti la Spoti
Starehe, Masoud Sanani, ambaye pia aliiongoza kamati hiyo mwaka uliopita.Kamati hiyo ya Tuzo
ilikutana mara ya mwisho hivi karibuni kwa ajili ya kupanga namna ya kuendesha tuzo hizo kwa mwaka
huu ili iwe bora zaidi ya ilivyokuwa mwaka jana.Pamoja na mambo mengine kamati ilikubaliana vyama
vya michezo vishirikishwe kwa kuviandikia barua ili vitume majina ya wanamichezo wao waliofanya
vizuri kwa mwaka 2011.Kutokana na hali hiyo kila chama cha michezo kitawasilisha  kwa kamati majina
matatu ya wanamichezo wake waliofanya vizuri mwaka jana kwa wanaume matatu na wanawake
matatu, ambao mmojawao atakuwa ndiye mshindi wa mchezo husika kwa mwaka jana.Pia kila mshindi
miongoni mwa wanamichezo hao atashiriki kuwania tuzo ya Mwanamichezo wa Bora wa Mwaka 2011.
Tarehe na mahali ambapo tuzo itafanyika itatangazwa wiki hii baada ya kumalizika vikao muhimu,
ambapo pia mdhamini wa tuzo atatajwa, ingawa TASWA inafungua mlango kwa kampuni zaidi
zijitokeze kudhamini kwa vile tuzo ya mwaka huu itakuwa ya aina yake.Kwa hiyo wafuatao ndio
wanaunda Kamati ya TASWA ya Kusimamia Upatikanaji wa Wanamichezo Bora wa Tanzania kwa
mwaka 2011, wengi wakiwa ni wale waliokuwepo mwaka uliopita..Mwenyekiti wa Kamati atakuwa
Sanan, ambaye ni Mhariri wa gazeti la Spotistarehe, Katibu wa kamati atakuwa Amir Mhando ambaye
ni Katibu Mkuu wa TASWA,  Mshauri wa Kamati atakuwa Juliana Yassoda ambaye ni Naibu Mkurugenzi
wa Idara ya Maendeleo ya Michezo. Pia Kamati itaomba Ofisa mmoja wa Baraza la Michezo la Taifa
(BMT) naye kuwa mshauri wa kamati.
Orodha kamili ya wajumbe ni
1.Amour Hassan-Mhariri Nipashe
2. Rashid Zahoro-Mhariri gazeti la Burudani
3. Alex Luambano-Clouds FM
4. Tulo Chambo-Mhariri Tanzania Daima
5. Mbonile Burton-HabariLeo
6. Chacha Maginga-TBC1
7.Frank Sanga-Mhariri Mwanaspoti
8. Michael Maurus-Super Star
9. James Range-Star TV
10.Editha Mayemba-Radio Tumaini
11. Said Kilumanga-Chanel Ten/Magic Radio
12.Rehule Nyaulawa-Mkurugenzi Times FM
13. Angel Akilimali-Meneja Vipindi Radio Uhuru
14. Masoud Sanan-Mhariri Spotistarehe
15. Amir Mhando-Katibu Mkuu TASWA
16. George John –Katibu Msiadizi TASWA
17.Patrick Nyembela-EATV
18: Juliana Yassoda-Naibu Mkurugenzi Idara ya Michezo
19. Luqman Maloto-Championi
20. Deo Rweyunga-Radio One
21. Andrew Kingamkono-Mhariri Mwananchi
22. Dominick Isiji-The African
23. Ofisa kutoka BMT
HABARI HII KWA HISANI YA BLOGU YA BIN ZUBEIRY NA MAMA PIPIRO

No comments:

Post a Comment