KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, May 3, 2012

Hakimu Simba na Yanga huyu hapa


SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limempanga mwamuzi Hashim Abdalla wa Dar es Salaam kuchezesha pambano la marudiano la ligi kuu ya Bara kati ya watani wa jadi, Simba na Yanga.
Hashim ni mwamuzi wa daraja la kwanza na ni mara yake ya kwanza kuchezesha mechi kati ya timu hizo kongwe nchini, ambayo kwa kawaida huvuta hisia za mashabiki wengi.
Ofisa Habari wa TFF, Boniface Wambura alisema mjini Dar es Salaam jana kuwa, Hashim atasaidiwa na Iddi Maganga na Omary Kambangwa. Mwamuzi wa akiba atakuwa Hamisi Chang’walu wote wa Dar es Salaam.
Pambano kati ya Simba na Yanga linatarajiwa kupigwa keshokutwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Katika mechi ya awali iliyochezwa mwishoni mwa mwaka jana kwenye uwanja huo, Yanga iliichapa Simba bao 1-0.
Wakati huo huo, klabu ya Simba imeamua kuwapatia wachezaji wake sh. milioni 35 kutokana na kuichapa Al-Ahly Shandy ya Sudan katika mechi ya michuano ya Kombe la Shirisho.

No comments:

Post a Comment