KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, January 4, 2012

KUMRADHI



Wapenzi wasomaji wa blogu hii ya Liwazozito, kwa takriban mwezi mmoja sasa sikuweza kuweka habari yoyote mpya kwenye blogu hii kwa sababu nilikuwa likizo ya mwaka kutoka kwa mwajiri wangu. Hivyo niliamua kwenda mapumziko nyumbani Tabora. Niliamua kupumzisha akili na mawazo nyumbani kwetu kwa sababu hiyo ndiyo maana halisi ya kuwa likizo. Unatakiwa upumzishe akili na mawazo kwa kufanya vitu tofauti na vile ulivyovizoea.

Nimerejea rasmi mjini Dar es Salaam, Januari 5, 2012 na nawaahidi kuendelea kuwapa habari mbalimbali kuhusu michezo na burudani pamoja na makala za kusisimua za mastaa wa michezo mbalimbali.

Bila kusahau, nawatakia wasomaji wapenzi wa blogu hii heri ya mwaka mpya na tumuombe Mola wetu aendelee kutuweka hai ili tuendelee kuwasiliana mara kwa mara kupitia blogu hii. Ahsanteni.

Ramoza.

No comments:

Post a Comment