KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, January 11, 2012

Mzee Kipara afariki


MMOJA wa waigizaji wakongwe wa maigizo na vichekesho nchini, Fundi Saidi ‘Mzee Kipara’ amefariki dunia.
Habari zilizopatikana mjini Dar es Salaam leo zimeeleza kuwa, Mzee Kipara alifariki dunia saa tatu asubuhi nyumbani kwake Kigogo.
Kwa mujibu wa habari hizo, Mzee Kipara alifikwa na mauti baada ya kuugua kwa muda mrefu maradhi mbalimbali, yakiwemo ya kuvimba miguu.
Mzee Kipara alijipatia umaarufu mkubwa kuanzia miaka ya 1970 alipokuwa akishiriki michezo ya kuigiza iliyokuwa ikirushwa hewani na Radio Tanzania Dar es Salaam.
Mkongwe huyo aliendelea kujizolea umaarufu baada ya kujitosa kwenye fani ya filamu, ambapo alishiriki kucheza tamthilia mbalimbali zilizokuwa zikiandaliwa na kikundi cha Kaole.

No comments:

Post a Comment