KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, January 5, 2012

Riyama aibuka na filamu kali



MWIGIZAJI na mtayarishaji maarufu wa filamu nchini, Riyama Ali yupo katika hatua za mwisho za maandalizi ya filamu yake mpya ya Likwata.
Riyama alisema mjini Dar es Salaam wiki hii kuwa, picha za filamu hiyo zinatarajiwa kupigwa ndani ya mji wa Dodoma, ambako ndiyo yanakotarajiwa kuwa makao makuu ya serikali.
Mwigizaji huyo alisema, filamu yake hiyo inatarajiwa kuwakutanisha wasanii kadhaa nyota na itarekodiwa katika vitongoji mbalimbali vya mji huo.
Kwa mujibu wa Riyama, Likwata ni jina la mmoja wa wasanii watakaocheza filamu hiyo, ambayo itakuwa ya kufungua mwaka 2012 kwake.
Mmoja wa washiriki wa filamu hiyo, Swebe Santana alisema baada ya kusoma maelezo yake, alivutiwa nayo na kukubali mara moja kushiriki kuicheza.
“Kaka ukiona msanii anakubali kuja kurekodi filamu mkoani, tambua kuwa filamu hiyo si mchezo,” alisema msanii huyo.
“Likwata ni filamu ya kipekee na ya aina yake, Riyama aliponifuata na kuniomba nishiriki kuicheza, nilimwomba ‘script’ nisome na niliposoma, niligundua kuwa filamu imetulia, ndio maana nipo hapa Dodoma,”alisema Swebe.
Washiriki wengine wa filamu hiyo ni Stara Thomas, Adam Melele, Zuber Mohamed ‘Niva’, Adam Kuambina, Hagy na baadhi ya wasanii kutoka Dodoma.
Riyama, ambaye ni mshindi wa tuzo za Risasi (Risasi Award 2005/2006), ndiye msanii pekee ambaye bado hajapotea katika tasnia ya filamu.
Baadhi ya filamu alizoshiriki kuzicheza ni Fungu la kukosa, Fake Promise, My Darling’, 'Simu ya Kifo’, ‘Darkness Night’, ‘Mwana Pango’, ‘Kolelo’,'Segito’, ‘Miwani ya Maisha’ na ‘Mzee wa Busara.

No comments:

Post a Comment