KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, January 9, 2012

UKWA: Nimepata mchumba





LAGOS, Nigeria
MWIGIZAJI machachari wa Nigeria, Osita Iheme, maarufu kwa jina la Ukwa, ametangaza kuwa naye amepata mchumba na wanatarajia kufunga ndoa hivi karibuni.
Ukwa ametoa taarifa hiyo siku chache baada ya swahiba wake mkubwa na mwigizaji mwenzake, Chinedu Idekieze ‘Aki’ kufunga ndio na Nneoma.
Hata hivyo, Ukwa hakuwa tayari kutaja jina la mchumba wake huyo, mwonekano wake ama taarifa zozote zaidi kuhusu kufunga naye ndoa.
Ukwa alisema amefurahishwa na uamuzi wa rafiki yake, Aki kufunga ndoa na kuongeza kuwa, ameamua kufuata nyayo zake.
“Nami nimepata mpenzi. Niko makini katika uhusiano wetu wa kimapenzi,”alisema Aki na kumtaka mwandishi wa mtandaji wa filamu za Kinigeria kuwa na subira kabla hajaweka mambo hadharani.
Ukwa pia alieleza kufurahishwa kwake na uamuzi wa serikali ya Nigeria kuwapa tuzo baadhi ya waigizaji nyota wan chi hiyo, akiwemo yeye.
“Ni jambo zuri na la kufurahisha kuwa miongoni mwa watu maarufu nchini Nigeria. Nilipokosa nafasi hii mwaka jana, niliwaeleza watu kwamba zamu yangu inakuja,”alisema mcheza filamu huyo.
“Na hatimaye zamu yangu sasa imefika. Nina furaha kubwa sana. Namshukuru Rais Goodluck Jonathan kwa kunipa heshima hii. Naahisi siwezi kumwangusha,”aliongeza.
Ukwa amecheza filamu zaidi ya 100 akishirikiana na Aki. Filamu yao ya kwanza iliyowapatia umaarufu inajulikana kwa jina la Aki na Ukwa.
Wachezaji filamu hao wawili wafupi na wenye vituko, kwa sasa ni miongoni mwa wasanii tajiri nchini Nigeria, wakiwa wanamiliki nyumba katika mini ya Aba, Enyimba na Abia na pia magari ya kifahari.
Ukwa anaishi Ogba, Ikeja nje kidogo ya Jiji la Lagos. Kwa sasa, wacheza filamu hao wamepanga kujenga jengo la pamoja katika mji huo.

1 comment: