KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, January 5, 2012

Sikuolewa na Aki sababu ya pesa-Nneoma



LAGOS, Nigeria
MKE wa mcheza filamu nyota wa Nigeria, Nneoma Ikedieze amesema hakuolewa na mumewe, Chinedu Idekieze ‘Aki’ kwa sababu ya pesa na umaarufu wake.
Nneoma, ambaye alifunga ndoa na Aki mwishoni mwa wiki iliyopita, alisema wiki hii mjini hapa kuwa, ameamua kuolewa na mcheza filamu hiyo kwa sababu ya mapenzi aliyonayo kwake.
Mwanadada huyo, ambaye ni mhitimu wa shahada ya mawasiliano ya umma, aliyoipata Chuo Kikuu cha Enugu alisema, alianza kuwa na uhusiano na Aki miaka mitatu iliyopita.
“Tulikutana Lagos. Tulifanyakazi pamoja. Siku zote nilizoea kumuona. Napenda staili ya maisha yake. Hivyo tulianza kuwa marafiki na kuanzia hapo ndipo safari yetu ilipoanza,”alisema Nneoma.
Alisema tangu alipokutana na Aki, aliweza kubaini mara moja kuwa ni aina ya mwanaume anayempenda kutokana na jinsi alivyo.
Alimwelezea Aki kuwa ni mwanaume mwenye akili na mtanashati na pia mwenye mapenzi ya kweli.
Nneona alisema wazazi wake hawakupatwa na mshangao wowote baada ya kuwaeleza kuhusu uamuzi wake wa kutaka kufunga ndoa na Aki.
“Baba yangu aliniambia niendelee na mipango yangu iwapo ndiye chaguo langu,”alisema mwanadada huyo, ambaye anamzidi Aki kwa umbo na urefu.
Nneoma alisema anampenda mno Aki kama alivyo na kusisitiza kuwa, kamwe hawezi kufanya hivyo kwa sababu ya pesa na umaarufu wake.
“Watu wanaweza kusema vyovyote wapendavyo. Ni kauli zisizokuwa na msingi wowote. Nimefunga ndoa na Chinedu Ikedieze, sikuolewa na Aki,”alisisitiza.
Alisema hakuna chochote, ambacho angependa kibadilike kwa Aki baada ya kufunga naye ndoa na kwamba, alivyo anatosha kwake.

1 comment:

  1. Congrats for that decision as I believe a good wife comes fro god and I wish you all the best in your new marriage.But the most important thing in marriage is respect to one another,honest,love and enduarance.
    Christopher' fro Kenya.
    Good bless you all.

    ReplyDelete