KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, January 5, 2012

Yanga yaiadhibu Kikwajuni



NaHamad Hija, Maelezo, Zanzibar

MABINGWA wa soka wa Tanzania Bara, Yanga jana waliona mwezi baada ya kuichapa Kikwajuni mabao 2-0 katika mechi ya michuano ya Kombe la Mapinduzi iliyochezwa kwenye Uwanja wa Amaan mjini hapa.

Ushindi huo ulikuwa wa kwanza kwa Yanga katika michuano hiyo iliyoanza kutimua vumbi mwishoni mwa wiki iliyopita. Katika mechi yake ya kwanza, Yanga ilichapwa bao 1-0 na Mafunzo.

Iliwachukua Yanga dakika 24 kuhesabu bao la kwanza lililofungwa na Jerry Tegete kwa shuti kali, ambali kipa wa Kikwajuni alishindwa kulizuia. Bao hilo lilidumu hadi mapumziko.

Zikiwa zimesalia dakika tano pambano hilo kumalizika, Yanga iliongeza bao la pili kupitia kwa mshambuliaji wake, Pius Kisambale.

Mashindano hayo ni sehemu ya maadhimisho ya sherehe za miaka 48 ya Mapinduzi ya Zanzibar zinazotarajiwa kufikia kilele Januari 12 mwaka huu.

No comments:

Post a Comment