KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, January 9, 2012

Omotola na wenzake wanusurika kufa baharini


LAGOS, Nigeria
MCHEZA filamu nyota wa kike nchini Nigeria, Omotola Jalade pamoja na mwongoza filamu, Teco Benson wamenusurika kufa baharini baada ya boti waliyokuwa wakisafiria kuzima ghafla.
Tukio hilo lilitokea hivi karibuni wakati Omotola, Benson pamoja na waigizaji wengine 22 pamoja na wapiga picha walipokuwa wakiigiza filamu ya Blood In The Lagoon.
Habari za uhakika kutoka eneo la tukio zimeeleza kuwa, boti hiyo ilikuwa imekodishwa na Benson kwa ajili ya kuwasafirisha waigizaji hao kurudi Lagos wakitokea kisiwa cha Victoria.
Kwa mujibu wa habari hizo, boti hiyo ilikwama ghafla ilipokuwa ikikaribia kisiwa hicho kilichopo kwenye bahari ya Atlantiki na kusababisha mtafaruku wa aina yake miongoni mwa waigizaji hao.
Vyanzo vya habari vimeeleza kuwa, kukwama kwa boti hiyo baharini kulitokana na kuishiwa mafuta kwenye tanki.
Akihojiwa kuhusu tukio hilo, Benson alisema halikuwa kosa lao, bali la wamiliki wa boti hiyo. Alisema waliishiwa mafuta wakati walipokuwa wakirejea kutoka kwenye eneo la kupiga picha za filamu yake mpya.
“Tulikodi boti kwa gharama kubwa, lakini pengine hawakutazama kiwango cha mafuta kilichokuwemo kabla ya kutusafirisha. Tulikuwa watu kama 22 kwenye boti,”alisema.
“Wakati tukio hilo lilipotokea, tulikuwa tukikaribia ubalozi wa Marekani na tulikuwa na wasiwasi huenda walinzi wake wangetushambuliaji kwa kuhisi sisi ni magaidi, lakini hakuna kilichotokea,”aliongeza.
Benson alisema wamiliki wa boti hiyo waliwasiliana na wenzake, ambao walifika na boti nyingine baadaye na kuwaondoa kwenye eneo hilo la hatari.
Kwa mujibu wa Benson, walidumu kwenye eneo hilo la bahari kwa muda wa kama dakika 45 kabla ya kuokolewa.
“Hakukuwa na cha zaidi, lakini wanawake waliokuwemo kwenye boti walionyesha hofu kubwa na kufikiri wanaweza kufa baharini. Tunamshukuru Mungu hakuna kibaya kilichotokea,”alisema.
“Lilikuwa tukio la kufurahisha, tulipiga picha za filamu ya Blood Ine Lagoon na kuhisi Lagoon alitaka damu zetu halisi,”aliongeza Benson huku akicheka.

No comments:

Post a Comment