KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Friday, January 27, 2012

MWASIKILI, NGELEJA NA MDEE BWANA!

NAHODHA wa timu ya soka ya taifa ya wanawake, Twiga Stars, Sophia Mwasikili akionyesha kitita cha sh. milioni saba, ambazo timu hiyo ilizawadiwa na wabunge kwa ajili ya malipo yao ya posho katika hafla iliyofanyika juzi kwenye uwanja wa Karume, Dar es Salaam.

WAZIRI wa Nishati na Madini, William Ngeleja (kushoto) akiteta jambo la Mbunge wa Kawe (CHADEMA), Halima Mdee kabla ya kuanza kwa mechi ya kirafiki kati ya timu ya wabunge na timu ya taifa ya wanawake, Twiga Stars, iliyochezwa juzi kwenye uwanja wa Karume, Ilala, Dar es Salaam. Twiga Stars ilishinda mabao 2-1.



No comments:

Post a Comment