KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, March 27, 2014

EMEKA IKE AKANA KUTENGANA NA MKEWE




LAGOS, Nigeria
KATIKA siku za hivi karibuni, kumekuwepo na uvumi kwamba, mwigizaji Emeka Ike na mkewe, wamekuwa katika msuguano mkali uliosababisha watengane.

Kwa mujibu wa habari hizo, mke wa Emeka alidai talaka kutoka kwa mumewe kutokana na kuchoshwa na tabia za mwigizaji huyo.

Habari hizo ziliendelea kueleza kuwa, kutokana na ndoa ya wawili hao kuvunjika, Emeka aliamua kuwachukua watoto wao wawili na kwenda nao Abuja, akimuacha mkewe akibaki na watoto wengine wawili mjini Lagos.

Hata hivyo, Emeka amekanusha vikali habari hizo na kuziita kuwa ni za uzushi.

Emeka ameandika kwenye mtandao wa facebook wiki hii: " Huu ni uzushi."

Mbali na kuandika maneno hayo, Emeka aliweka picha aliyopiga pamoja na mkewe na watoto wao wanne.

No comments:

Post a Comment