KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Saturday, March 15, 2014

DORIS: NITAKWENDA KOKOTE MUNGU ATAKAKONIONGOZA



LAGOS, Nigeria
IMEPITA miaka miwili tangu ndoa ya mchezaji filamu nyota wa Nigeria, Doris Simon na mumewe, Daniel Ademinokan, ilipovunjika. Tangu wakati huo, Doris ameamua kuishi pweke, japokuwa mtoto wake wa kiume waliyezaa, Daniel anaishi na mzazi mwenzake.

Akihojiwa na mtandao mmoja wa habari nchini Nigeria hivi karibuni, Doris alizungumzia mambo mbalimbali kuhusu kuvunjika kwa ndoa yake.

"Chochote kingeweza kwenda mrama. Chochote kingeweza kusababisha moto mahala kokote. Huwezi kujua nini kinaweza kutokea dakika moja ijayo. Tunajaribu kuweka mambo sawa, lakini Mungu ndiye mwenye uamuzi wa mwisho,"amesema Doris.

"Ni kweli, mambo mengi hutokea maishani na unaweza kuendelea kujiuliza maswali mengi kuhusu kilichotokea na kusababisha jahazi liende mrama. Kama utaendelea kuwa katika hali hiyo, huwezi kusonga mbele kwa sababu kila kitu kinachotokea, Mungu ameweka mkono wake. Kuna sababu kwa nini mambo yanakuwa hivi na imeandikwa kwamba itatokea hivyo,"aliongeza

Doris amesema tangu ndoa yake ilipovunjika, amekuwa akiulizwa maswali mengi. "Watu wananiuliza, 'Doris unadhani utaendeleaje na maisha yako? Utafanya nini ili kusonga mbele'"

"Nimeamua kuyapuuza maswali hayo na kusonga mbele. Ningejikita kujibu maswali hayo, ningechanganyikiwa na kupandwa na hasira,"alisema.

"Wapo watu waliokuwa wakitaka kunicheka, hivyo niliona ni vyema niwaache wabaki na mshangao. Ndio sababu nimeamua kusonga mbele na maisha yangu,"alisisitiza mwanadada huyo mwenye umbo na sura jamali.

Alipoulizwa iwapo atafikiria kuolewa tena, Doria alisema: "Siwezi kuelewa. Lakini siwezi kusema lolote kwa sababu mimi ni binadamu. Ninaweza kujitosa katika penzi jingine. Lakini kwa sasa acha nifanye kile ninachoendelea kukifanya. Popote ambako Mungu ataniongoza, nitakwenda."

No comments:

Post a Comment