KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, March 23, 2014

YANGA YAIPUMULIA AZAM, LEO NI SIMBA NA COASTAL UNION



MABINGWA watetezi wa ligi kuu ya soka ya Tanzania Bara, Yanga jana waliibuka na ushindi mnono wa mabao 3-0 dhidi ya Rhino Rangers katika mechi iliyopigwa kwenye Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora.


Ushindi huo umeiwezesha Yanga kuwa na pointi 43 baada ya kucheza mechi 20, ikiwa nyuma ya vinara, Azam kwa tofauti ya pointi moja. Azam inatarajiwa kushuka tena dimbani leo kuvaana na JKT Oljoro.

Mashujaa wa Yanga katika mechi hiyo walikuwa Jerry Tegete, aliyefunga bao la kwanza dakika ya 26, Simon Msuva, aliyefunga la pili dakika ya 67 ma Hussein Javu, aliyefunga dakika ya 90.

Wakati huo huo, Simba leo itakuwa na kibarua kigumu itakapomenyana na Coastal Union kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment