KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, March 20, 2014

D'BANJ: BABA HAKUTAKA NIWE MWANAMUZIKI




LAGOS, Nigeria
LICHA ya kupata mafanikio makubwa kimuziki, mwanamuziki nyota wa Nigeria, D'banj amefichua kuwa baba yake hafurahishwi na kazi yake hiyo.

"Baba yangu aliniasa tangu nikiwa mdogo kwamba nisijihusishe na mambo ya muziki,"alisema D'banj alipohojiwa na mtandao mmoja wa Nigeria.

"Hata hivi sasa, amekuwa akinieleza: 'Una hakika fani ya muziki ni sahihi kwako?'"Alisema mwanamuziki huyo.

D'banj amepata mafanikio makubwa kimuziki tangu alipoibuka na kibao cha Oliver Twist na ameuza nakala zaidi ya milioni 11 za albamu zake.

Alipoulizwa ni kazi ipi, ambayo baba yake angependa kumuona akiifanya, alisema: "Kazi nyingine yoyote mbali na muziki."

Kwa mujibu wa D'banj, baba yake amekuwa na wasiwasi kuwa, umaarufu alionao kutokana na muziki, huenda ukayaharibu maisha yake.

"Ana wasiwasi iwapo nitaendelea kupata mafanikio haya kwa muda mrefu,"alisema mwanamuziki huyo, ambaye amewahi kuhusishwa kimapenzi na wasanii mbalimbali maarufu wa Kinigeria.

"Amekuwa akiniambia: 'Nilipokuwa na umri kama wako, tayari nilishaoa na kukupata wewe. Ni lini utaweka mambo sawa na kufunga ndoa?'" Alisema D'banj.

Mwanamuziki huyo alisema moja ya malengo yake ni kushinda tuzo ya muziki ya Grammy kwanza, lakini iwapo malaika atampitia karibu, anaweza kubadili mpango wake huo.

No comments:

Post a Comment