KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, March 20, 2014

'WALIDHANI WANANOIIMALIZA, KUMBE WANANIPA UMAARUFU'


LAGOS, Nigeria
BAADA ya kukaa kimya kwa muda mrefu, mcheza filamu machachari wa Nigeria, Biola Ige, ameamua kufunguka na kuzungumzia picha zake zilizosambazwa kwenye mitandao.

Picha hizo zilizozua gumzo kubwa miongoni mwa mashabiki wa filamu wa Nollywood, zinamwonyesha Biola akiwa amekumbatiana na Muna Obiekwe huku mwanaume huyo akiwa ameweka mikono yake kwenye matiti ya binti huyo.

Katika taarifa yake aliyoitoa kwa vyombo vya habari wiki hii, Biola ameamua kuweka mambo hadharani kwa kusema, picha hiyo alipigwa wakati wa kutayarisha filamu ya Pregnant Hawkers.

Biola amemponda mtu aliyeisambaza picha hiyo kwenye mitandao kwa malengo tofauti na kusema, alichokifanya ni kumtangaza na kumpa umaarufu.

"Picha inayozungumzwa na kuzua maswali, ilipigwa katika eneo tulilokuwa tukipiga picha za filamu ya Pregnant Hawkers, ambayo nilicheza kama mwanamke aliyekuwa katika hali ya mapenzi na mwanaume,"amesema Biola.

"Picha za filamu hii zilipigwa miaka miwili iliyopita. Picha iliyosambazwa kwenye mitandao kwa sasa ni picha iliyopigwa kwenye eneo tulilotumia kupiga picha za filamu hiyo, hakuna kingine,"aliongeza msanii huyo.

"Iwapo utatazama filamu hiyo, utaona kwamba hakuna kingine kilichojitokeza katika filamu hiyo zaidi ya ukweli kwamba, nilikuwa nikicheza nafasi niliyopangiwa,"alisema binti huyo katika taarifa yake hiyo.

"Nimepitia matatizo mengi mwaka huu, ikiwa ni pamoja na kumpoteza mama yake na kuugua kwa muda mfupi. Picha hiyo kutoka kwenye filamu niliyocheza miaka miwili iliyopita, haiwezi kunipa wasiwasi wowote,"alisisitiza binti huyo.

Biola amesema ataendelea kucheza filamu nyingi zaidi katika nafasi mbalimbali kwa lengo la kuwaburudisha mashabiki wake.

No comments:

Post a Comment