KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, March 27, 2014

KUMBE ZACK ORJI NI MWANAMUZIKI




LAGOS, Nigeria
WATU wengi wanamtambua Zack Amaefula Orjioke, kuwa ni mmoja wa wacheza filamu nyota na wakongwe nchini Nigeria.

Mkongwe huyo, ambaye ni maarufu zaidi kwa jina la Zack Orji, amecheza filamu nyingi na kujipatia sifa na umaarufu mkubwa kwa mashabiki wa fani hiyo nchini Nigeria.

Kumbe Zack anacho kipaji kingine cha ziada. Nacho ni muziki. Amepanga kuingia studio hivi karibuni na kurekodi wimbo wake wa kwanza.

Akihojiwa na gazeti la Sun la Nigeria wiki hii, Zack alisema ameamua kujitosa kwenye fani hiyo kwa vile anacho kipaji kingine cha ziada.

Kwa mujibu w a Zack, kibao chake hicho kinajulikana kwa jina la Cradles of Greatness, ambacho kinaelezea mambo mbalimbali kuhusu nchi yake ya Nigeria.

Katika moja ya beti za wimbo huo, Zack ameandika maneno yafuatayo:

"Oh Nigeria, nchi ya asili ya mababu zetu, tunajivunia asili yetu, tunakupenda. Japokuwa tunatofautiana katika makabila na lugha, bado tuko pamoja. Tunajivunia nchi ya asili yetu. Nchi yenye ndoto na nafasi nyingi. Alama ya umoja wetu. Nchi ya uhuru wetu."

No comments:

Post a Comment