KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, March 31, 2014

KOMBE LA NSSF LAANZA KWA KISHINDO



 Mgeni rasmi, Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudencia Kabaka akisalimiana na wachezaji wa Azam TV
 Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudencia Kabaka akirusha mpira kimiani wakati alipokuwa akifungua michuano ya netiboli.
 Waziri Kabaka akisalimiana na mwamuzi, Hassan Isihaka aliyechezesha mechi ya soka kati ya Habari Zanzibar na New Habari
Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudencia Kabaka akisalimiana na wachezaji wa Habari Zanzibar
HABARI Zanzibar jana ilianza vyema michuano ya soka ya Kombe la Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), baada ya kuibugiza New Habari mabao 4-1 katika mechi iliyochezwa kwenye uwanja wa klabu ya Sigara, Chang'ombe, Dar es Salaam.

Mabao ya Habari Zanzibar yalifungwa na Yussuf Chuma aliyefunga matatu bna Amir Suleiman wakati bao la kujifariji la New Habari lilifungwa na Florian Masinde.

Katika netiboli, Jambo Leo ilianza michuano hiyo kwa kishindo baada ya kuibugiza Wizara ya Habari mabao 60-8 wakati Azam TV iliicharaza TSN mabao 18-13.

Michuano hiyo ilifunguliwa na Waziri wa Kazi na Ajira, Gaudencia Kabaka, ambaye alivitaka vyombo vya habari kuitumia kujenga ushirikiano na kuimarisha umoja miongoni mwao.

Waziri Kabaka pia alivitaka vyombo hivyo vya habari kuepuka kuwatumia wachezaji wasio waajiriwa kwa sababu kufanya hivyo ni kuondosha maana ya mashindano hayo.

No comments:

Post a Comment