KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, March 20, 2014

MWANANGU ANANIFANYA NIONE FAHARI-CLARION




LAGOS, Nigeria
MCHEZA filamu mkongwe wa Nigeria, Clarion Chukwura, amesema anaona fahari kuwa mama wa muongozaji wa video za muziki nchini humo, Clarence Peter.

Clarion, amesema anaona fahari kwa kijana wake huyo kutokana na kuwa miongoni mwa watu waliochangia kuufanya muziki wa Nigeria upate sifa na umaarufu kimataifa.

Peter amechangia kuipaisha fani ya muziki wa Nigeria kutoka na ubunifu wake katika kutengeneza video zenye mvuto.

Kwa sasa, Peter anaheshimika kama mtayarishaji na muongozaji bora wa video za muziki kupitia lebo yake ya Capital Hill Records.

"Naona fahari kumzungumzia Peter popote ninapokwenda,"alisema Clarion, ambaye amecheza filamu zaidi ya 100 za Kinigeria na kujipatia umaarufu mkubwa.

Peter, hawafanyi wazazi wake pekee waone fahari ju yake, bali pia taifa zima la Nigeria. Ametayarisha na kuongoza video za muziki za wasanii mbalimbali wapya na wakongwe.

No comments:

Post a Comment