KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, March 26, 2014

STELLA AFUNGA AKAUNTI ZAKE ZOTE ZA FACEBOOK


LAGOS, Nigeria
MCHEZA filamu mwenye mvuto nchini Nigeria, Stella Damasus, ameamua kufunga akaunti zake za facebook kutokana na kuingiliwa na baadhi ya watu wenye dhamira mbaya.
Stella alisema wiki hii mjini hapa kuwa, baadhi ya watu wamekuwa wakitumia akaunti zake hizo kuwalaghai mashabiki wake na kujipatia pesa kwa njia ya udanganyifu.
Uamuzi huo wa Stella, umekuja siku chache baada ya mcheza filamu mwingine nyota wa Ghana, Yvonne Nelson, kuwataka wamiliki wa mtandao wa Twitter kuwadhibiti watu wanaoingilia akaunti yake.
"Napenda kuwafahamisha kwamba, kuanzia leo nafunga akaunti zangu zote za facebok. Ninamaanisha hivyo. Tafadhali sambaza ujumbe huu na kuwaeleza marafiki kwamba, baada ya leo, yeyote atakayejiita Stella Damasus kwenye facebook, siye mimi.
"Nataka kujilinda na kujiweka kwenye mtazamo bora, hasa baada ya baadhi ya matapeli kuanza kutumia akaunti zangu kukusanya pesa kutoka kwa watu wasiokuwa na hatia, ambao wanataka kujitosa kwenye fani ya uigizaji. Ni bora nipoteze akaunti zangu za facebook kuliko kuwaacha watu wafikirie kwamba naweza kufanya kitu kama hicho. Nawapenda na Mungu awabariki," ameeleza Stella.

No comments:

Post a Comment