KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, March 17, 2014

JK AIPATIA SIMBA MIL 30



RAIS Jakaya Kikwete, ameipa klabu ya Simba sh. milioni 30 ili kupata hati ya kujenga uwanja wake wa soko ulioko Bunju, Dar es Salaam.

Akizungumza katika mkutano wa marekebisho ya katiba ya klabu hiyo jana, Mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage alisema, Rais Kikwete, alitoa fedha hizo jana alipokutana naye Ikulu, Dar es Salaam.

Rage alisema Rais Kikwete alimwambia fedha hizo ametoa kama mwanamichez , anayependa kuona mchezo wa soka nchini unapata mafanikio kwa klabu kumiliki uwanja wake.

Alisema uzalendo wa Rais Kikwete, ni mfano bora wa kuigwa kwa kuwa amefanikisha jambo kubwa lililokuwa muhimu kwa ustawi wa Simba.

"Rais ameonyesha ni jinsi gani ana mapenzi na maendeleo ya michezo, hilo ni jambo kubwa,hivyo klabu ya Simba inamshukuru na tunaahidi kukamilisha ujenzi wa uwanja huo haraka iwezekanavyo,"alisema.

Mwenyekiti huyo wa Simba alisema, fedha hizo zitatumika kulipa hati ya uwanja na itakabidhiwa katika mkutano mkuu wa uchaguzi utakaofanyika Mei 4 mwaka huu.

Alisema ahadi ya ujenzi wa uwanja huo iko pale pale na utajengwa ndani ya siku 100 kama ilivyoahidiwa na maandalizi yanaendelea.

No comments:

Post a Comment