KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Saturday, March 15, 2014

'NAPENDA KUOLEWA NA MWANAUME TAJIRI'


LAGOS, Nigeria
MCHEZA sinema mwenye mvuto nchini Nigeria, Lizzy Gold Onuwaje amesema kamwe hawezi kuolewa na mwanaume masikini.

Lizzy, ambaye alitwaa taji la mrembo wa Jimbo la Delta 2006, amesema anapenda kuolewa na mwanaume tajiri na mwenye uwezo mkubwa kipesa.

Mrembo huyo wa filamu, alisema hayo wiki hii alipohojiwa na gazeti la Vanguard la Nigeria.

"Napenda wanaume, ambao wapo tayari kutumia pesa na sio wanaume bahiri,"alisema mrembo huyo mwenye tabasamu mwanana.

"Uhusiano wa kimapenzi kati yangu na mpenzi wangu wa zamani, haukuvunjika kwa sababu ya mimi kuamua kuwa mwigizaji Ukweli ni kwamba hakuwa na pesa, hivyo nikaamua kuachana naye,"alisema mrembo huyo.

"Niliachana naye mwaka jana kwa sababu hakuwa na pesa au kitu chochote, ambacho kingeweza kumuingizia pesa,"aliongeza.

"Napenda mwanaume anayejali. Unapaswa kuwa tajiri, mzuri, unayejali na mwenye mapenzi ya kweli. Baadhi ya wanaume ni matajiri, lakini mabahiri. Kuwa tajiri na uwe tayari kutumia pesa. Iwapo nitakwambia nahitaji kitu chochote, acha nipate ishara. Napenda ishara,"alisema.

Lizzy alisema mwanaume asiye na pesa, asijisumbue kumpigia simu ana kuzipenda picha zake. Alisema anapenda mno pesa na kusisitiza kwamba, kamwe hawezi kuolewa na mwanaume masikini.

"Nahitaji mwanaume tajiri. Pesa zina maana kubwa kwangu. Fedha zinanipa uhai,"alisema mwanadada huyo huku akiangua kicheko.

Lizzy alikwenda mbali zaidi kwa kusema, mwanaume asiye na utajiri, kamwe hawezi kuwa na mvuto kwake.

"Ninaposema tajiri, sina maana ya wanaume aina ya 'Yahoo' kwa sababu sio wachapakazi. Nataka mwanaume, ambaye ni mchapakazi na tajiri. Kwa sasa nimeridhika na mwanaume niliyenayo na sifikirii kuachana naye kwa ajili ya mwanaume mwingine,"aliongeza msisitizo.

No comments:

Post a Comment