KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, March 17, 2014

UCHAGUZI MKUU SIMBA MEI 4


UCHAGUZI mkuu wa klabu ya Simba umepangwa kufanyika Mei mwaka huu mjini Dar es Salaam.

Uamuzi wa kupanga tarehe hiyo ulifikiwa katika kikao cha kamati ya utendaji ya Simba kilichofanyika mjini Dar es Salaam juzi chini ya Mwenyekiti wa klabu hiyo, Ismail Aden Rage.

Katika kikao hicho, kamati hiyo pia ilifanya uteuzi wa wajumbe wa kamati ya kusimamia uchaguzi huo itakayoongozwa na mwanasheria, Damas Ndumbaro.

Makamu mwenyekiti wa kamati hiyo ni Salum Madenge, katibu ni Issa Batenga, katibu msaidizi ni Khalid Kamguna. Wajumbe wengine ni Kassim Dewji, Juma Simba na Amin Bakhressa.

No comments:

Post a Comment