KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, March 27, 2014

DESMOND: SIWEZI KUACHA UIGIZAJI

LAGOS, Nigeria
KUMEKUWEPO na uvumi kwamba, mwigizaji na mtayarishaji mahiri wa filamu wa Nigeria, Desmond Elliot, anataka kuachana na fani hiyo ili ajitose kwenye siasa.

Baadhi ya mitandao ya kijamii na magazeti ya Nigeria, yaliripoti hivi karibuni kuwa, Elliot anataka kuipa kisogo fani hiyo ili aweze kupata muda wa kutosha katika masuala ya siasa.

Hata hivyo, mwigizaji huyo mwenye mvuto na mshindi wa tuzo za AMVCA, amekanusha taarifa hizo kwa kusema si sahihi.

Eliiot alisema wiki hii mjini hapa kuwa, ni kweli anataka kuwania nafasi ya kisiasa katika uchaguzi mkuu wa 2015, lakini hawezi kuacha uigizaji.

Msanii huyo, ambaye amekuwepo kwenye fani ya uigizaji kwa karibu miaka 12 sasa, alisema: "Siwezi kuacha uigizaji. Kama wamesema hivyo, siyo kweli. Sielewi wameyapata wapi maneno hayo."

No comments:

Post a Comment