KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, March 31, 2014

SIMBA, YANGA ZACHEZEA VICHAPO LIGI KUU



MABINGWA watetezi wa ligi kuu ya soka ya Tanzania Bara, Yanga na watani wao wa jadi, Simba jana walichezea vichapo kutoka kwa timu za Mgambo JKT na Azam.


Wakati Yanga ilichapwa mabao 2-1 na Mgambo kwenye Uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga, watani wao Simba walichezea kichapo hicho kutoka kwa Azam kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Matokeo hayo yaliiwezesha Azam kuzidi kujichimbia kileleni mwa ligi hiyo, ikiwa na pointi 53 baada ya kucheza mechi 22 wakati Yanga inaendelea kushika nafasi ya pili ikiwa na pointi 46.

Mabao ya Azam yalifungwa na Khamis Mcha na John Bocco dakika ya 16 na 56 wakati bao la Simba lilifungwa na Uhuru Selemani dakika ya 45.

Kwa upande wa Yanga, kipigo ilichokipata kimefifisha matumaini ya timu hiyo kutetea taji hilo msimu huu.

Iliwachukua Mgambo dakika moja kuhesabu bao la kwanza lililofungwa na Full Maganga kwa shuti la mbali lililomshinda kipa Juma Kaseja.

Bao la kusawazisha la Yanga lilifungwa kwa njia ya penalti na nahodha Nadir Haroub 'Cannavaro dakika ya 52 baada ya beki mmoja wa Mgambo kuunawa mpira ndani ya eneo la hatari.

Mgambo iliongeza bao la pili dakika ya 63 lililofungwa na Malima Busungu kwa njia ya penalti baada ya kukwatuliwa na beki mmoja wa Yanga ndani ya eneo la hatari.

No comments:

Post a Comment