KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Monday, March 17, 2014

WACHEZAJI YANGA WANUSURIKA KATIKA AJALI


WACHEZAJI wa timu ya soka ya Yanga wamenusurika kifo baada ya basi walilokuwa wakisafiria kupata ajali walipokuwa njiani wakirejea Dar es Salaam kutoka Morogoro.

Ajali hiyo ilitokea jana saa tatu asubuhi katika eneo la Mikese, timu hiyo ilipokuwa ikitoka Morogoro kucheza mechi ya ligi kuu ya Tanzania Bara dhidi ya Mtibwa Sugar.

Katika mechi hiyo iliyochezwa juzi kwenye Uwanja wa Jamhuri, Morogoro, timu hizo zilishindwa kutambiana baada ya kutoka suluhu.

Ofisa Habari wa Yanga, Baraka Kizuguto, alisema kwa njia ya simu kutoka eneo la ajali kuwa, ajali hiyo ilitokea baada ya basi la klabuhiyo lenye namba za usajili T 916 CCS kuacha njia na kutumbukia kwenye mtaro.

Kizuguto alisema msafara wao ulinusurika kifo, baada ya basi hilo kukita katika eneo lenye majani nje kidogo ya barabara.

Alisema hakuna mchezaji au kiongozi aliyeumia kutokana na ajali hiyo na kwamba waliendelea na safari baada ya kupata basi lingine ya kampuni ya Abood.

Kwa mujibu wa Kizuguto, wachezaji na viongozi wa timu hiyo walilazimika kutokea madirishani kutokana na mlango wa basi kuegemea kwenye ardhi.

No comments:

Post a Comment