KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Friday, March 4, 2011

Kelvin adai yeye si mtukutu

MCHEZA filamu machachari wa Nigeria, Kelvin Ikeduba amesema yeye si mtu mbaya kama watu wengi wanavyomfikiria.
Kelvin alisema mwishoni mwa wiki iliyopita mjini hapa kuwa, kuna tofauti kubwa kati ya tabia yake halisi na zile anazoigiza kwenye filamu mbalimbali.
Mwigizaji huyo alisema, licha ya kucheza filamu nyingi akiwa kijana mtukutu, hiyo si tabia yake na haina maana kwamba ni kijana mbaya.
“Kelvin aliye nyuma ya kamera ni kijana wa kawaida tu. Lakini angeweza kuwa kijana mbaya iwapo anataka iwe hivyo,”alisema.
“Inawezekana ni kwa sababu ya mwonekano wangu, nimecheza filamu nyingi nikiwa kijana mtukutu, lakini hii haina maana kwamba mimi ni mtu mbaya,”alisisitiza.

No comments:

Post a Comment