KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Friday, March 4, 2011

Ramsey Nouah awa mchungaji!


MSHINDI wa tuzo ya mwigizaji bora wa kiume wa filamu wa mwaka 2010, Ramsey Nouah amesema haoni tatizo kwake kuigiza nafasi ya mchungaji katika filamu ya ‘The Perfect Church’.
Akizungumza mjini hapa mwishoni mwa wiki iliyopita, Ramsey alisema awali, hakupenda kuigiza nafasi hiyo, lakini baadaye alijipa moyo na kuona ni changamoto mpya kwake.
Ramsey, ambaye amecheza filamu hiyo kama Mchungaji Benson, alisema ameifurahia nafasi hiyo kwa vile imemtofautisha na filamu nyingi alizowahi kucheza, hasa zinazohusu masuala ya mapenzi.
Mtunzi wa filamu hiyo, Wale Adenuga alisema, ana hakika itapata mafanikio makubwa sokoni kwa vile wametumia utaalamu wa hali ya juu katika kuitengeneza.
Mbali na Ramsey, wasanii wengine walioshiriki kucheza filamu hiyo ni pamoja na Funke Akindele, Hakeem na Ngozi, ambao wameigiza kama bibi na bwana Ojo.

No comments:

Post a Comment