KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Friday, March 4, 2011

Funke Akindele aporwa


KUNDI la majambazi mwishoni mwa wiki iliyopita lilivamia hoteli ya Imperial ya mjini Lagos na kupora vitu kadhaa na mamilioni ya fedha kutoka kwa wateja, akiwemo mcheza filamu machachari, Funke Akindele.
Watu walioshuhudia tukio hilo walisema, Funke pamoja na watu wengine wa familia yake, walikuwemo kwenye hoteli hiyo wakati wa tukio hilo, lakini hakuna aliyejeruhiwa.
Kwa mujibu wa mashuhuda hao, kabla ya uvamizi huo, majambazi hao walipiga risasi hewani kutishia watu na baadaye walianza kuulizia mahali alipokuwepo mwigizaji huyo.
Funke alithibitisha kutokea kwa tukio hilo, lakini alikataa kulizungumzia kwa undani zaidi ya kumshukuru Mungu kwamba alikuwa salama.
Chanzo cha habari kilisema jumla ya fedha na vitu vilivyoibwa na majambazi hao vinakadiriwa kuwa na thamani ya zaidi ya Naira milioni mbili za Nigeria.

No comments:

Post a Comment